· Yana ukubwa ekari 7,700 katika vijiji viwili tu
· Aagiza Afisa Ardhi arudishwe kutoka Rorya kusaidia uchunguzi
WAZIRI
MKUU Kassim Majaliwa ameagiza kufutwa mara moja umiliki wa mashamba
makubwa 11 yenye ukubwa wa ekari 7,700 kwenye vijiji vya Kasharazi na
Rwakalemera wilayani Ngara Kagera, ambayo hayana hati na yametelekezwa.
Ametoa
agizo hilo leo asubuhi (Jumatano, Machi 16, 2016) wakati akizungumza
na wakazi wa vijiji vya Kasulo na Rwakalemera katika kata ya Kasulo
wilayani Ngara akiwa njiani kuelekea mkoa wa Geita.
Waziri
Mkuu alilazimika kufanya mkutano huo mapema asubuhi baada ya kuamua
kuitisha uongozi wa wilaya ya Ngara ufike kwenye mkutano huo ili kujibu
kero za wananchi waliosimamisha msafara wake jana wakati akielekea Ngara
mjini.
Uamuzi
huo unafuatia hatua ya Waziri Mkuu kumwita kwenye mkutano huo Afisa
Ardhi na Maliasili wa Wilaya, Bi. Betty Munuo ili aeleze chanzo cha
mgogoro wa ardhi katika vijiji hivyo.
Bi.
Munuo ambaye amehamishiwa wilaya hiyo Agosti, mwaka jana, alisema
aliyakuta malalamiko hayo na amefanya uchambuzi wa majina ya wamiliki
wote wa mashamba na walikuwa wanapanga kuwapatia notisi ili wajieleze.
Katika
orodha yake, Bi. Munuo alitaja wamiliki 18 wa mashamba makubwa lakini
kati yao ni wamiliki saba tu ambao mashamba yao yana hati lakini matatu
ndiyo yameendelezwa na manne hayajaendelezwa.
Mashamba
yaliyoendelezwa yanatumika kwa kilimo, ufugaji na shule. Nayo
yanamilikiwa na Dayosisi ya Rulenge (shamba na. 606 lenye ekari 161 liko
Mbuba); Dario Zakaria (shamba na. 639 lenye ekari 282 liko Nyakariba)
na Masista wa Mt. Fransisco (shamba na. 234 lenye ekari 759 liko
Kasulo).
0 comments: