Thursday, March 27, 2014

Siasa za kupata katiba mpyaTanzania zapamba moto

at 3:43:00 AM  |  No comments


Hata hivyo uteuzi huo utakaoambatana na wenyeviti wengine waliochaguliwa kwenye kamati 12 ulichukuliwa na baadhi ya wajumbe kwa hisia tofauti za kutoaminiana kwa kazi wanayokwenda kuifanya mbele yao ya kuandika katiba ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.

Wabunge wakiwa ndani ya bunge maalumu la katiba mjini Dodoma, Tanzania Wabunge wakiwa ndani ya bunge maalumu la katiba mjini Dodoma, Tanzania

 Mjumbe mwingine John Mnyika alisema kamati hiyo itaendelea kulalamikiwa  sio tu kwa kukosa uwiano wa pande mbili za muungano bali hata katika upande mmoja wa muungano kukosa sura kabisa ya uwakilishi jambo  ambalo alisema halieleweki.

Hata hivyo Profesa Lipumba  wa chama cha CUF alikanusha kuwa yeye ni mwenyekiti wa kundi la Umoja wa Katiba ya Wananchi-UKAWA  na kusema kuwa  mwenyekiti wake ni Bw. Freeman Mbowe  wa chama cha CHADEMA. Lipumba alisema katika hali inavyokwenda  katika bunge hilo ni wazi kabisa kwamba hakuna nia njema ya  kupata katiba ya wananchi.

Aidha wajumbe wengine walipinga uteuzi huo ambao una wawakilishi kutoka chama tawala cha CCM na kumshauri mwenyekiti huyo wa bunge kufikiria upya juu ya uteuzi alioufanya bila kuegemea vyama vya kisiasa.
Kwa upande mwingine mmoja wa wajumbe aliyesimama kwa muda mrefu kuomba muongozo wa mwenyekiti bila ya mafanikio Bw. Ezekiel Oluochi amedai kuwa randama ya pili ya rasimu ya katiba, ambayo ndiyo yenye uchambuzi wa kina wa mambo yanayobishaniwa hawana wajumbe wengi wa bunge hilo maalum la katiba.

Share
Posted by Unknown
About the Author

Write admin description here..

0 comments:

Text Widget

Blogger templates. Proudly Powered by Blogger.