NiceMediaWorks
Home
Posts
Email
MATUKIO
HABARI
MAGAZETI
MAKALA
BURUDANI
AFYA
PRODUCTION
INJILI
Style Icons
MAWASILIANO
Top 10 List
Wednesday, January 27, 2016
MAAMUZI YA KESI YA KUPINGA MATOKEO JIMBO LA TARIME VIJIJINI YAAHIRISHWA
at 12:25:00 PM | 
No comments
Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza leo imeahirisha Kesi ya Kupinga Matokeo ya Uchaguzi Mkuu Jimbo la Tarime Vijijini uliofanyika Novemba 25,2015. Kesi hiyo ilifunguliwa aliekuwa Mgombea wa Jimbo hilo kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Christopher Ryoba Kangoye akiiomba Mahakama kutengua Ushindi wa Mgombea wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema John Heche aliechaguliwa kuwa mbunge wa Jimbo hilo kwa kuwa uchaguzi huo haukuwa wa huru na haki.
Kesi hiyo ambayo ilianza kusikilizwa January 19,2015 chini ya Jaji wa Mahakama hiyo Mhe.Lameck Mlacha leo imeahirishwa hadi kesho January 28,2015 majira ya saa nane mchana itakapotolewa maamuzi yake.
Mjibu maombi katika kesi hiyo (John Heche) anawakilishwa na Mawakili Tundu Lisu (leo hakuwa Mahakamani) pamoja na Paul Kipeja (alikuwepo Mahakamani).
Baada ya Kesi hiyo Kuahirishwa, Katibu wa Chadema Mkoani Mara Mwl.Chacha Heche (Pichani Juu anaehojiwa) ameiomba Mahakama kutoa maamuzi ya Kesi hiyo ili kuwapunguzia gharama kwa kuwa ambazo zinajitokeza wakiwa Jijini Mwanza kufuatilia maamuzi ya kesi hiyo.
Barnabas Nyangi Lubare ambae ni mmoja wa Wakazi wa Jimbo la Tarime akihojiwa na Wanahabari baada ya kesi kuahirishwa amesema kuwa wanatarime vijijini wana imani na Mahakama na kwamba kesi hiyo ni sehemu ya changamoto kwa mbunge wao na kwamba wembe ni ule ule wa kushinda kuanzia jimboni hadi Mahakamani.
Barnabas Nyangi Lubare ambae ni mmoja wa Wakazi wa Jimbo la Tarime akihojiwa na Wanahabari baada ya kesi kuahirishwa.
Paul Kipeja ambae ni Wakili upande wa Mjibu Maoni akizungumza na wanahabari baada ya Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza kuahirisha kutoa Maamuzi ya kesi ya Kupinga Matokeo Jimbo la Tarime Vijijini.
Anasema kama ilivyokuwa katika Kesi ya Kupinga Matokeo ya Uchaguzi Jimbo la Bunda Mjini iliyofunguliwa na Wapiga kura wa Jimbo hilo dhidi ya Esther Bulaya (Mbunge), ndivyo itakavyokuwa hata katika Jimbo la Tarime Vijijini kwa maana ya mteja wao (John Heche) kushinda kesi inayomkabiri.
Share
MATUKIO
Posted by Unknown
About the Author
Write admin description here..
«Newer Post
Older Post»
0 comments:
About Me
Unknown
View my complete profile
NiceMedia. Powered by
Blogger
.
BOFYA HAPA LIVE NICEMEDIA RADIO
Radio ya Injili inayoburudisha na Kuelimisha
Popular
Recent
Comments
Tags
Popular Posts
South Africa links Rwanda diplomats to attacks
Kenya anti-terrorism squad gets $735 a month
Waislamu waendelea kuuawa na Anti-Balaka CAR
kuzisha hati Milioni moja wakimbia machafuko Sudan Kusiniwa
PITIA MAGAZETI YA LEO ALHAMISI DECEMBER 15, 2016
Labels
Afya
BURUDANI
Favourite
Gear
HABARI
HABARI ZA INJILI
HIVI PUNDE
MAGAZETI
MAKALA
MATUKIO
nice studio
SIASA
slider
TANGAZO
Nice Media work Tz
Latest tweets
Latest Videos From NiceMedia Prod.
Search
BLOG RAFIKI
Udaku Special
MillardAyo
Jiachie
Text Widget
© 2013
NiceMediaWorks
.
Woo Themes
converted by
Bloggertheme9
Blogger templates
. Proudly Powered by
Blogger
.
0 comments: