NiceMediaWorks
Home
Posts
Email
MATUKIO
HABARI
MAGAZETI
MAKALA
BURUDANI
AFYA
PRODUCTION
INJILI
Style Icons
MAWASILIANO
Top 10 List
Wednesday, March 26, 2014
Watu 11 wafariki katika milipuko ya mabomu Nigeria
at 2:19:00 AM | 
No comments
Watu wasiopungua 11 wakiwemo maafisa watano wa polisi wameuawa katika miripuko miwili ya mabomu iliyotokea katika eneo lililoathiriwa na machafuko huko kaskazini mashariki mwa Nigeria. Miripuko hiyo ya mabomu ilitokea huko Maiduguri makao makuu na mji mkubwa zaidi katika jimbo la Borno kwa kupishana dakika kadhaa. Msemaji wa polisi Gideon Jibrin ameeleza kuwa raia watatu waliuawa baada ya gari moja kuripuka na maafisa watano wa polisi walifariki dunia baada ya bomu la pili lililokuwa limetegwa kwenye gari la polisi kuripuka dakika kumi baada ya mripuko wa kwanza. Msemaji huyo wa polisi ameongeza kuwa hata hivyo bado hawajafahamu iwapo watu wengine watatu waliouliwa kwenye mripuko wa pili walikuwa ni wategaji mabomu hayo au la. Mbali na miripuko hiyo ya jana, watu wengine 20 waliuliwa pia Jumapili wiki hii katika mripuko uliotokea kwenye soko moja huko Bama katika jimbo la Borno.
Share
Posted by Unknown
About the Author
Write admin description here..
«Newer Post
Older Post»
0 comments:
About Me
Unknown
View my complete profile
NiceMedia. Powered by
Blogger
.
BOFYA HAPA LIVE NICEMEDIA RADIO
Radio ya Injili inayoburudisha na Kuelimisha
Popular
Recent
Comments
Tags
Popular Posts
South Africa links Rwanda diplomats to attacks
Kenya anti-terrorism squad gets $735 a month
Waislamu waendelea kuuawa na Anti-Balaka CAR
kuzisha hati Milioni moja wakimbia machafuko Sudan Kusiniwa
PITIA MAGAZETI YA LEO ALHAMISI DECEMBER 15, 2016
Labels
Afya
BURUDANI
Favourite
Gear
HABARI
HABARI ZA INJILI
HIVI PUNDE
MAGAZETI
MAKALA
MATUKIO
nice studio
SIASA
slider
TANGAZO
Nice Media work Tz
Latest tweets
Latest Videos From NiceMedia Prod.
Search
BLOG RAFIKI
Udaku Special
MillardAyo
Jiachie
Text Widget
© 2013
NiceMediaWorks
.
Woo Themes
converted by
Bloggertheme9
Blogger templates
. Proudly Powered by
Blogger
.
0 comments: